Frashvortex

Monday

knowledge half

Am happy for this situation that make me to be hire for that time even  if i will be silent for a long time bcoz of life consurming at this time guys.....!
welcom to our blog and share other to ready read News from prince mkolera.....!

Tuesday

JINSI NDUGU ZETU WA KENYA WANAVYO PATA SHIDA

 HIVI NDIVYO WANAJESHI WA JESHI LA KENYA WANAVYO PATA TABU.
 TUWAOMBEE KWA MUNGU ILI AWANUSURU NA JANGA HILI ZITO LINALO WAKABILI.
 SIKIA KWA JIRANI TU,LAKINI ISITOKEE KWAKO MAANA NI BALAAAAAA.....!
 WANA EAST AFRICA,TUWAOMBEE KWA HALI NA MALI NDUGU ZETU JAMANI.
 HIVI NDIVYO ILIVYO KUWA HALI YA WENZETU WAKENYA,TABU NYINGI WANAZIPATA,HURUMA YA MUNGU IWAFIKIE JAMANI.....!
 ANGA LIMECHAFUKA KWELI KWELI JAMANI,NI JANGA LA TAIFA HILI.
 TAZAMA TABU WANAZO PATA WANAJESHI JAMANI ,KAMA TUKO SOMALIA.......!
Nikiwa kama kiongozi wa BLOG hii, napenda kutoa pole za dhati kwa wana -EAST AFRICA GUYS wote kwa JANGA hili linalo wakabili wenzetu wa KENYA tangu siku ya JUMAMOSI mpaka leo hii.pia pole nyingi ziende kwa wale wote walio ondokewa na ndugu/wazazi/watoto na wengineo katika janga hili.
Tuko pamoja nao kwa kila hatua na tunwaombea kwa MUNGU awape nguvu na imani katika kipindi hiki kigumu sana.

                                                          AMEN:

Wednesday

BINTI MACHOZI

HEY GUYS WATCH THIS VIDEOS,BEATIFULL LADY,GOOD SONG AND BETTER VIDEO.....!
BY:ICTS-MKOLERA.

Sunday

HIZI NDIZO NDEGE KUBWA DUNIANI ZILIZOTENGENEZWA KWA TECHNOLOGIA YA HALI YA JUU (ANTONOV 225 AN)


Hizi ndizo Ndege kubwa Duniani zinazobeba mizigo na zimetengenezwa kwa Technologia ya hali ya juu, Ndege hizi zote zimetengezezwa nchini (Ukrainian) na kampuni moja inaitwa {Soviet Union's Antonov Desig}
 SIFA ZAKE



  • Crew: 6
  • Length: 84 m (275 ft 7 in)
  • Wingspan: 88.4 m (290 ft 0 in)
  • Height: 18.1 m (59 ft 5 in)
  • Wing area: 905 m2 (9,740 sq ft)
  • Aspect ratio: 8.6
  • Empty weight: 285,000 kg (628,317 lb)
  • Max takeoff weight: 640,000 kg (1,410,958 lb)
  • Fuel capacity: 300000 kg
  • Cargo hold – volume 1,300m3, length 43.35m, width 6.4m, height 4.4m
  • Powerplant: 6 × ZMKB Progress D-18 turbofans, 229.5 kN (51,600 lbf) thrust each


    UFANYAJI KAZI WAKE
     
  • Maximum speed: 850 km/h (528 mph; 459 kn)
  • Cruising speed: 800 km/h (497 mph; 432 kn)
  • Range: 15,400 km (9,569 mi; 8,315 nmi) with maximum fuel; range with maximum payload: 4,000 km (2,500 mi)
  • Service ceiling: 11,000 m (36,089 ft)
  • Wing loading: 662.9 kg/m² (135.8 lb/sq ft)
  • Thrust/weight: 0.234

JESHI LETU LA JWTZ NA MONUSCO LAFANIKIWA KUITEKA NGOME KUU YA WAASI WA M23


ASKARI wa Umoja wa Mataifa wanaolinda amani nchini DR Congo (MUNUSCO), wakiongozwa na vikosi vya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) vimefanya shambulizi la nguvu katika eneo la  Kibati (Nyirangongo Territory, Goma, Eastern DRC), eneo hilo ndiyo iliyokuwa ngome kuu ya waasi wa M23

Shambulio hilo kubwa na la kwanza kufanywa na vikosi vya Umoja wa Mataifa limekuja siku moja, baada ya Askari wa JWTZ kuuawa na waasi wa M23 katika shambulio lao la juzi wakati vikosi vya UN vilipokuwa katika ukaguzi wa maeneo yenye usalama katika mji wa Goma.

Askari huyo wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, JWTZ Khatibu Mshindo aliuawa kwa kupigwa bomu juzi na waasi wa M23 kwenye Mji wa Goma ulioko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo baada ya kuzuka mapigano makali.
 
Mshindo aliuawa baada ya mapigano makali yanayoendelea katika Mji wa Goma, ambapo ilielezwa kwamba Askari wa M23 waliwazidi ujanja majeshi ya Umoja wa Mataifa wanaolinda amani nchini Congo.Wakati Mshindo ambaye alikuwa miongoni mwa askari wa Tanzania wanaounda Jeshi la Umoja wa Mataifa akifikwa na mauti, wapiganaji wengine 10 walijeruhiwa.

Waasi wa M23 waliokuwa Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamesema kuwa watasitisha mapigano, kufuatia makabiliano makali na wanajeshi wa serikali wanaoungwa mkono na wanajeshi wa Umoja wa Mataifa.
 
Wakati M23 wakidai kwamba watasitisha mapigano hayo, taarifa zaidi zinaeleza kwamba Majeshi ya UN yanayo ongozwa na majeshi ya Tanzania yamefanya mashambulizi makali ya mizinga pamoja na Askari wa Miguu wakipanda milima na kuwasambaratisha waasi wa M23 na kuteka ngome yao.
  NEWS AND PICTURE BY MKOLERA

RWANDA YAPELEKA WANAJESHI 1700 KUWASAIDIA WAASI WA M23 BAADA YA KUELEMEWA NA JWTZ ( MONUSCO)

KIKUNDI cha waasi cha M23 kinachopambana na jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), kimeripotiwa kupigwa vibaya na kutikisa nguvu za kikundi hicho kutokana na baadhi ya wapiganaji wake kuripotiwa kupoteza maisha.
 
Mapigano baina ya M23 na Jeshi la Serikali ya DRC linalosaidiwa na Kikosi Maalumu cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa (MONUSCO), yameibuka upya ndani ya wiki hii.
 
Habari za kiintelijensia  zinasema kuwa, kutokana na shambulio hilo, Serikali ya Rwanda imelazimika kuingilia kati kusaidia waasi hao kwa kupeleka bataliani mbili zenye jumla ya askari 1,700 huko DRC, ili waweze kukabiliana na nguvu ya majeshi ya JWTZ, DRC, Monusco na Brigedi ya Majeshi ya Kulinda Amani ya Umoja wa Mataifa yenye mamlaka ya kujibu mapigo (FIB).

Kwa mujibu wa vyanzo hivyo vya habari, Rwanda imepeleka bataliani hizo mbili zenye askari 850 kila moja saa 48 zilizopita na kwamba wamevuka mpaka kuingia DRC katika eneo la Kibumba, lakini wanashindwa kusonga mbele.
 
Habari zaidi zinasema sababu ya Rwanda kupeleka askari wake hao ni kusaidia M23 ambao walipigwa sana Agosti 23 na 27, mwaka huu katika eneo la vilima vya Kibati na  kuikimbia ngome yao.
 
“M23 walitandikwa sana Agosti 23 na 27 katika eneo la vilima vya Kibati, na kulazimika  kuikimbia ngome yao, ndio maana sasa hivi Rwanda imepeleka batalioni zao kuwapa nguvu, lakini wanashindwa kusonga mbele maana hawajielewi kwa sababu ya kipigo walichopata,” kilisema chanzo kimoja cha habari.
 
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo vya habari, eneo la Kibati ndilo eneo kubwa la M23 ambalo wamekuwa wakitumia kuhifadhi silaha zao za kivita, lakini wakati wa mapambano majeshi ya JWTZ , DRC, MUNUSCO na FIB yalisambaratisha kabisa ngome hiyo ya waasi.
 
FIB inaundwa na askari wengi wa Afrika Kusini na Tanzania. Habari zaidi zinasema kwa sasa majeshi ya DRC, Monusco na FIB yanawasubiri kwa hamu askari hao wa Rwanda kuingia uwanja wa vita ili kukabiliana nao kama walivyokabiliana na waasi wa M23.
 
“Taarifa tulizonazo hivi sasa Rwanda inajiuliza iwapo isonge mbele kupambana au irudi nyuma, ikifikiria pia kipigo walichopata M23,” kilisema chanzo kimoja cha habari. 

Inaelezwa kwamba, kutokana na kipigo walichopata M23 siku chache zilizopita kimepelekea Rwanda kujikuta ikikiri na kusema ukweli juzi kuwa inakisaidia kikundi hicho cha waasi.
by:mkolera

Thursday

BREAKING NEWS: RAPPER LANGA KILEO A,K,A LANGA AFARIKI DUNIA

Msanii wa hiphop Tanzania, Langa Kileo a.k.a Langa amefariki dunia leo (13th) muda mfupi uliopita  katika hospitali ya muhimbili jijini Dar.Akizungmza na Clouds Fm, Afisa uhusiano wa hospitali ya taifa ya Muhimbili, Ameniel Aligaesha, amethibitisha kwamba msanii Langa, amefariki dunia leo hii saa kumi na moja za jioni, baada ya kufikishwa hospitalini hapo juzi jioni.
hata hivyo uongozi wa Muhimbili hauna uwezo wa kusema kilichomuua Langa, kutokana na maadili ya kazi zao, bali ndugu wa  marehem.
Kifo cha Langa kimetufika ikiwa ni siku 17 tu tangu kufariki kwa msanii mwingine wa hiphop na freestyle master Albert Mangwea A.k.a Ngwea.
Mungu ailaze roho ya matehem mahali pema peponi

Tuesday

MWILI WA MAREHEMU ALBERT MANGWEHA A.K.A NGWAIR WAPOKEWA NYERERE AIRPORT NA UMATI WA WATANZANIA

Wasanii,waandaji,mashabiki na wadau wa muziki wa kizazi kipya Tanzania wameungana kupokea mwili wa marehemu Albert Mangwear pale Air Port Mchana wa leo.Albrt Mangweha "Ngwair" alifariki Jumanne iliyopita 28/5/2013 huko Afrika Kusini.



Wednesday

soory

DAAAAH....! SAMAHANINI SANA WANA EAST AFRICA KWA KILI AMBACHO NILIPOST MIDA FULAHI,KIUKWELI SIKUWA SAWA WADAU WANGU.

Tuesday

ANNOUNCEMENT

NDUGU ZANGU WAPENDWA,WADAU WA EAST AFRICA,SOTE TUKO SAFARINI KUELEKEA KWA MUNGU BABA MWENYE ENZI YOTE.
TUNACHO PASWA KWA SASA NI KUJIULIZA JINSI SAFARI YETU ITAKAVYO KUWA,WAKATI GANI NA MAHARI GANI,JE ITAKUWA KAMA YA BROTHER WATU NGWEAR AMA SHARO,N.K. KWETU WADAMU NI WAKATI WA MAJONZI SANA KWA KUONDOKEWA NA MSANII AMBAE TULIMPENDA SANA ;LAKINI MUNGU KAMPENDA ZAIDI YETU ,KWAHIYO HATUNA BUDI KUMWOMBEA APUMZIKE KWA AMANI HUKO ALIKO TANGULIA.
NASI TUKO NYUMA YAKE...................................!
                                                                            MKOLERA


Kifo cha Ngwair: picha waliyopiga siku ya mwisho, update ya hali ya mwenzie, M2-The-P

Kwa mujibu wa mtandao wa TeenTZ: Marehemu Albert Mangwea “Ngwair” alikua na msanii mwenzake wa bongo flavor ajulikanae kama M2-THE-P miongoni mwa wasanii waliokuwa marafiki wa kundi la CHAMBER SQUAD.

Habari zinasema kua hali ya M2-THE-P sio nzuri na yuko mahututi katika chumba maalumu (I.C.U) ambapo madaktari wamethibitisha kua matumaini ni hafifu ya uhai wake. “hali yake sio nzuri, tumemuwekea mashine ya kupumua na yuko kwa uangalizi wa kina kwa muda wa masaa sita nbaada ya hapo tutaweza kusema nini hatima yake kwa sasa ni hayo tu” – Daktari amenukuliwa.
Source:
BY:MKOLERA

Hapa Ndipo Mwili wa Marehemu albert Mangwea Ulipohifadhiwa Kwenye Hii Hospitali ya Helen Joseph




Ngwea amefariki dunia jana asubuhi katika moja ya vitongoji vya jiji la Johannesburg na baadaye wenzake walimkimbiza katika Hospitali ya St Helen Joseph.R.I.P
By:MKOLERA

Soma Kisa na Chanzo Cha Kifo cha Msanii Albert Mangwea Kwa Mujibu wa Mtoa Report Aliekuwa South Africa


 Msanii wa Bongo Fleva Albert Mangwair a.k.a Ngwair amefariki dunia akiwa nchini Afrika Kusini.

Taarifa zinasema Kwamba
Ngwea akiwa na msanii M to the P jana
south africa.mtu wa karibu anasema
walitakiwa kurudi dar leo lakini
waliwakuta wamezima kwenye room
wote wawili baada ya kuji overdose
madawa ya kulevya na M to the P yupo
hoi hospitali.
by:MKOLERA

Saturday

BAADA YA MAHOJIANO,MAKOSA YALIYO MNYIMA ZAMANA LEMA HAYA HAPA.......!

Mambo yaliyomfanya Mbunge wa arusha Godbless Lema akamatwe na kunyimwa dhamana jioni hii ni haya yafuatayo baada ya kuongea na Mwanasheria wa Lema wakili Humphrey Mtui

i)Kosa la kwanza ni kuwaambia wanafunzi wa chuo cha uhasibu alipoenda kuwatuliza kuwa ‘dhambi kubwa kuliko zote ni woga ‘.Haki hutafutwa na kupiganiwa ikiwa jambo unalipigania ni la msingi na linafaa kupiganiwa(Worth fighting for)

ii)Kosa la pili ni pale alipotamka kuwa ‘’Tumemtafuta mkuu wa mkoa juu ya Matatizo yenu na mlivyoshuhudia hapa amechukua muda mrefu na kuingia kama vile anaingia kwenye send-off.Hawa ndiyo viongozi wetu ambao hawajali matatizo ya wananchi’’Kwa hiyo huo ni uchochezi

iii)Kosa la Tatu ni pale alipotamka kuwaambia wanafunzi kuwa ‘’Mimi Mbunge wenu nipo sambamba nanyi hadi mpate haki yenu na ikiwa mkuu wa mkoa hatakuja hapa kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa mkoa nitawaongoza hadi ofisini kwake ili mpate majibu na haki yenu kwani ni haki yenu ya msingi kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo niliapa kuilinda Bungeni na pia inaruhusiwa kwa mujibu wa kikanuni na kifalsafa katika utekelezaji wa utawala bora wa kidemokrasia ambao msingi wake ni kusikilizwa na kulinda haki za binadamu’’Huu nao umeitwa kwamba ni uchochezi.

Sasa haya maneno hapo juu ndiyo yaliyosababisha jeshi la polisi kuvamia nyumbani kwake usiku wa manane na kuzua taharuki maeneo hayo na ndani ya nyumba yenye ndugu jamaa na hata mtoto mwenye miezi mitano huku polisi wakitumia nguvu na kukiuka sheria

Huo umeitwa uchochezi baada ya mkuu wa mkoa kumtumia ujumbe wa mkononi kupitia simu yake kupitia namba 0752960276 aliyotishia kumbambikizia kesi anayoitaka yeye.

Sasa hayo waliyoita makosa ya uchochezi ndiyo yaliyomnyima haki ya dhamana leo.tutafakari kama Arusha itatawalika kwa hali hii.

Hebu tupime makosa hayo matatu kama yanaweza ku-justfy mambo yote yaliyotokea
.
BY:MKOLERA.

Friday

SHEREHE ZA MUUNGANO





Hivi ndivyo sherehe za maazimisho ya miaka 49 ya MUUNGANO  zilivyo fana katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam,sherehe hizo zilizo ongozwa na mkuu wa majeshi MH:JAKAYA MRISHO KIKWETE.
Hizi baadhi ya picha,Ndege za kivita zikiwa zinapita katika anga la TANZANIA,JESHI LA WANANCHI ,WANANCHI pamoja na WAGENI WAALIKWA KUTOKA NCHI JIRANI.
                                     %MKOLERA%

MAAZIMISHO YA MIAKA 49 YA MUUNGANO .

 Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mwasisi namba moja na Hayati Abeid Aman Karume Mwasisi namba mbili wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kuunda Taifa la Tanzania
Leo Watanzania wote tunauenzi na kuukumbuka Muungano wetu wa Watanganyika na Wazanzibari, Muungano huu sasa umefikisha miaka 49 bila kutetereka ingawa kuna baadhi ya watu wanajaribu kuugusa kwa namna moja au nyingine kwa maslahi ya watanzania au yao binafsi, udini umekuwa suala zito katika muungano mpaka imefikia mapadri kupigwa risasi na kumpekekea mmoja wao kufariki dunia. Pia kuna watu wengine wanaubeza muungano kutokana na kuwa na maslahi yaho binasfi katika suala la muungano. 

Lakini kwa kutambua umuhimu wa jamii yoyote ile inapoungana tunaamini lazima umoja huo utakuwa na faida kama usemi wa wahenga unavyosema kidole kimoja akivunji chawa, pindi vitakapokuwa viwili ndio vitakapo weza kumuangamiza chawa huyo "UMOJA NI NGUVU UTENGANO NI UDHAIFU" kama watanzania wote tutatambua maana ya misemo yote hiyo, dhahiri hatutataka muungano huu uvunjike.

Tunaamini yapo mapungufu baadhi katika Muungano huu, la msingi ni kuweza kuangalia ni jinsi gani tunaweza kuyaboresha hayo mapungufu yaliyopo na watanzania wote kwa ujumla wetu tukafaidika na matunda ya Muungano wetu, napenda kuungana na Mh. Rais Kikwete katika Hotuba yake pale alipokuwa anawaapisha viongozi na wajumbe wa Tume ya kuangalia na kusikiliza maoni ya Katiba mpya ya kuwahasa mapema wale wote watakaowanahusika na mchakato huu kuwaomba na kuwasisitiza kuhusu Muungano maoni yawe ni jinsi gani tutauboresha muungano wetu na Sio suala la kuhoji Muungano uwepo au usiwepo, napenda kumpongeza sana kwa hili.

Mimi kama mtanzania halisi na ambaye ninaipenda nchi yangu napenda kumpongeza sana Mh. Rais na watanzania wote kwa ujumla wetu na hasa wale ambao wanaolitakia mema taifa letu.

"MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRIKA"