Frashvortex

Friday

MH. MIZENO PINDA AZINDUA RASMI RIPOTI YA IDADI YA WATU NA MAKAZI

Waziri Mkuu wa Tanzania MIZENGO PINDA leo amezindua rasmi ripoti ya idadi ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012 katika ngazi za Mikoa,Wilaya,Kata na Shehia, ambapo katika ripoti hiyo takwimu zinaonyesha kuwa Mkoa wa DAR ES SALAAM umeongoza kwa kuwa na watu Milioni 4.3 likiwa ni ongezeko la zaidi ya asilimia 5.5.
Aidha katika ripoti hiyo Mkoa wa MWANZA umeshika nafasi ya pili kwa kuwa na jumla ya Watu Milioni 2.7, sawa na ongezeko la asilimia 4 .3 kulinganisha na takwimu za sensa ya watu na makazi ya mwaka 2002, huku mkoa wa mpya wa KATAVI ukitajwa kuwa ndio mkoa wenye idadi ndogo zaidi ya watu kwa kuwa na watu laki Tano na Elfu Sitini pekee.
Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa ripoti hiyo Waziri Mkuu PINDA, amewataka watendaji wote wa Serikali katika ngazi za Mkoa na Wilaya kuhakikisha wanaongeza jitihada za utendaji wao.Katika hatua nyingine PINDA ametoa rai kwa Watanzania kuzingatia mfumo wa uzazi kwa Mpango ili kuipunguzia serikali mzigo.
Kwa upande wake Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar ambaye pia ni Kaimu Mwenyekiti wa Sensa ya Watu na Mkazi mwaka 2012, BALOZI SEIF ALLY IDDI amesema matokeo hayo yameibua changamoto nyingi.Matokeo ya jumla ya sensa ya watu na Makazi kwa mwaka 2012 yalizinduliwa rasmi Desemba 31 mwaka jana na Rais wa Tanzania Dokta JAKAYA KIKWETE na kuonyesha kuwa idadi ya watu TANZANIA imeongezeka na kufikia Milioni 44.9.
Sensa ya kwanza Tanzania ilifanyika mwaka 1910,huku Sensa nne za Mwisho zikifanyika baada ya Uhuru katika miaka ya 1967, 1978, 1988 na 2002,ambapo Kulingana na sensa ya mwisho iliyofanyika mwezi Agosti mwaka 2002, idadi ya watu Tanzania ilikuwa Milioni 34,4

No comments:

Post a Comment