Katika taarifa kwa taifa, makamu wa rais wa Venezuela Nicholas Marduro
ametangaza kufariki dunia kwa rais Hugo Chavez, 58, kufuatia kuugua muda
mrefu maradhi ya Saratani. Rais Chavez ametoweka katika hadhira ya nchi
hiyo kwa muda mrefu ambapo alikuwa anapokea matibabu nchi jirani ya
Cuba.
Alirejea , mjini Caracas mnamo Februari 18 kwa mara ya kwanza tangu
maradhi yake yamzidie ambapo alipelekwa hospitali ya kijeshi kuendelea
kupokea matibau. Hata hivyo maelezo zaidi hayakutolewa juu ya afya yake.
Waandamanaji waliandamana katika mji mkuu Caracas mwishoni mwa juma
wakidai kuwa watu wa Venezuela wanapaswa kupewa habari zaidi kuhusu afya
ya rais wao.
Bwana Chavez amekua uongozini nchini Venezuela kwa miaka 14 na
anatazamiwa kuleta mageuzi makubwa yaliyolenga zaidi kuimarisha maisha
ya raia wa pato la chini.
Ujumbe wa Jeshi
Taarifa kutoka kwa jeshi imesema kuwa wataendelea kuilinda hadhi ya nchi
na kuimarisha usalama. Pia jeshi limeahidi kuendelea kuwa waaminifu kwa
makamu wa rais Nicholas Marduro na wakatoa wito kwa raia kuwa watulivu.
No comments:
Post a Comment